Msichana wa miaka 16 nchini Afrika Kusini amejishindia zawadi ya maonyesho ya Google kwa kutumia maganda ya chungwa kutengeza kifaa kinachosaidia udongo kuhifadhi maji.
Kiara Nirghin aliwashinda wanafunzi wengine duniani kwa kujipatia ufadhili wa masomo wenye thamani ya dola 50,000 kwa ''kukabiliana na kiangazi kupitia chungwa''.
Kazi yake inajiri kufuatia kiangazi ambacho kinaendelea kuathiri Afrika Kusini.
Image captionMaganda ya chungwa yamshindia tuzo la Google
Manchester United wameondoka kwenye mkia kundi lao la ligi ndogo ya Ulaya, Europa League, baada ya kupata ushindi dhidi ya Zorya Luhansk.
Zlatan Ibrahimovic alifunga bao la pekee dakika ya 69, baada ya kombora la nguvu mpya Wayne Rooney kugonga mlingoti wa goli.
Hilo ndilo bao la kwanza la Ibra katika mechi tano, na lilitokana na kombora la kwanza la United lililolenga goli kwenye mechi hiyo.
United walitawala pakubwa mchezo huo uliochezewa Old Trafford, ingawa Sergio Romero alihitajika kufanya kazi ya ziada kuzima kombora la Paulinho muda mfupi kabla ya Ibrahimovic kufunga.
Mashetani hao Wekundu walitarajiwa kufanya vyema Europa League lakini walianza kampeni yao kwa kulazwa 1-0 na klabu ya Feyenoord ya Uholanzi mechi yao ya kwanza.
United sasa wamo nambari tatu kundini, wakiwa na alama sawa na Feyenoord na moja nyuma ya viongozi Fenerbahce wa uturuki ambao watazuru Old Trafford 20 Oktoba.
Leicester walicharaza Porto bao moja kwa bila mechi yao ya kwanza nyumbani katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya na kuendeleza mwanzo wao mwema katika dimba michuano hiyo mikuu ya Ulaya.
Islam Slimani, ambaye ana sifa nzuri ya kuwafunga Porto alipokuwa akichezea Sporting Lisbon, alifunga bao lake kwa kichwa dakika ya 25 kutokana na krosi ya Riyad Mahrez.
Nguvu mpya wa Porto Jesus Corona alifunga mlingoti kwa kombora lake lakini Leicester walikwamilia uongozi wao na wakaondoka na ushindi.
Slimani alinunuliwa na Leicester £29m siku ya mwisho sokoni. Ana sifa za kuwahangaisha Porto akiwa Sporting Lisbon hivi kwamba alikuwa amepewa jina la utani "the Dragon Slayer" (Mwuaji wa Zimwi)
Leicester wanaongoza Kundi F wakiwa alama mbili mbele ya FC Copenhagen walio nambari mbili.
Klabu hizo mbili zitakutana tarehe 18 Oktoba.
Leicester walioshangaza wengi kwa kushinda ligi kuu Uingereza msimu uliopita, wameanza vibaya msimu Ligi ya Premia, ambapo wameshindwa mechi tatu kati ya sita walizocheza kufikia sasa. Walifungwa mabao manne na Liverpool na Manchester United.
Image copyrightGETTY IMAGESImage captionLiverpool wamefanikiwa kushinda mechi nyingi ngumu ugenini
Meneja wa Liverpool, Jurgen Klopp amesema bado kuna nafasi ya kuimarika kama kikosi chake kinataka kupigania taji la Ligi Kuu ya Uingereza msimu huu hata baada ya kuanza vyema kampeni yao.
Liverpool ambao mara ya mwisho kutwaa ubingwa wa ligi ilikuwa mwaka 1990, waliicharaza Hull City kwa mabao 5-1 Jumamosi iliyopita na kupaa hadi mpaka nafasi nne katika msimamo, wakiwa nyuma ya vinara Manchester City kwa alama tano.
Liverpool wameshinda mechi ngumu za ugenini dhidi ya Arsenal na Chelsea huku wakiwababua mabingwa Leicester City kwa mabao 4-1 msimu huu.
Mechi pekee waliyopoteza ni ile waliyofungwa na Burnley.
Akihojiwa, Klopp amesema ni kweli kwa sasa wanacheza vizuri lakini bado kuna nafasi ya kuimarika ili waweze kuendeleza wimbi lao la ushindi.
Kiungo wa Manchester City, Yaya Toure amesema wachezaji na mashabiki wanaweza kuumia kufuatia hatua ya Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kuvunja kikosi kazi kilichoundwa kwa ajili ya kupambana na vitendo vya ubaguzi wa rangi katika soka.
Toure mwenye umri wa miaka 33, alikuwa mmoja wa wajumbe katika kikosi kazi hicho kilichoundwa mwaka 2013 kusaidia kutokomeza ubaguzi.
Katibu mkuu wa FIFA, Fatma Samba Diouf Samoura amesema kikosi kazi hicho kilikuwa na kazi maalumu ambayo tayari wameimaliza.
Hata hivyo, hatua hiyo imekosolewa vikali na wadau mbalimbali, akiwemo Toure ambaye alifanyiwa vitendo vya kibaguzi na mashabiki wa CSKA Moscow Octoba mwaka 2013.
Nyota huyo wa zamani wa kimataifa wa Ivory Coast amesema hatua hiyo ya FIFA itaweza kuwaumiza mashabiki na wachezaji kama mipango sahihi isipowekwa.
Rais wa Tanzania John Magufuli amewafuta kazi maafisa wawili wakuu wa serikali mkoani Kagera kutokana na tuhuma za kufungua akaunti iliyofanana na ile ya kukusanya pesa za kusaidia waathiriwa wa tetemeko la ardhi.
Add caption
Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Bw Amantius Msole na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba Bw. Steven Makonda.
Taarifa kutoka ikulu imesema kiongozi huyo amechukua hatua hiyo baada ya kubaini kuwa wamefungua akaunti nyingine kwa jina "Kamati Maafa Kagera" kwa lengo la kujipatia fedha.
Rais Magufuli ameagiza vyombo vya dola vichukue hatua dhidi ya wote waliohusika katika njama za kufungua akaunti hiyo.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa naye amemsimamisha kazi Mhasibu Mkuu wa Mkoa wa Kagera Bw. Simbaufoo Swai kutokana na kuhusika katika njama hizo.
Hatua hiyo imechukuliwa baada ya Rais kupokea msaada wa Shilingi milioni 545 kutoka kwa Waziri Mkuu wa India Narendra Modi za kusaidia waathiriwa wa tetemeko hilo la ardhi lililotokea 10 Septemba, 2016.
Bw Majaliwa ametoa wito kwa wananchi na taasisi mbalimbali kuendelea kuchangia misaada kwa ajili ya walioathirika kwa kutumia akaunti rasmi ya "Kamati Maafa Kagera".
Kundi la wachunguzi wa kimataifa waliochunguza kutunguliwa kwa ndege ya shirika la Malaysia Airlines safari nambari MH17 mashariki mwa Ukraine mwaka 2014 wamesema kombora lililotungua ndege hiyo lilirushwa kutoka maeneo yaliyodhibitiwa na waasi walioungwa mkono na Urusi.
Kundi hilo, likitoa ripoti yake ya awali ya uchunguzi nchini Uholanzi, limesema kombora lilirushwa kutoka karibu na kijiji cha Pervomaiskiy.
Wachunguzi hao pia wamesema kombora hilo aina ya BUK lililoundiwa nchini Urusi pamoja na mtambo wa kurusha kombora hilo, vilitolewa Urusi na vilirejeshwa huko siku iliyofuata.
Wachunguzi hao, ambao wamekuwa wakikusanya ushahidi kwa lengo la kubaini uwezekano wa kufunguliwa kwa kesi ya jinai, wanasema wanachunguza watu karibu mia moja waliohusishwa na shambulio hilo ingawa si kwamba wote ni wachunguzi.
Kundi hilo la wachunguzi wa kimataifa liliongozwa na wataalamu kutoka Uholanzi, wakishirikiana na wataalamu wa mashtaka kutoka Australia, Ubelgiji, Malaysia na Ukraine.
Watu wote 298 waliokuwa kwenye ndege hiyo aina ya Boeing 777 iliyokuwa safarini kutoka Amsterdam kuelekea Kuala Lumpur walifariki baada ya ndege hiyo kuanguka eneo la Grabovo jimbo la Donetsk .
Uchunguzi wa awali ulioongozwa na Bodi ya Usalama ya Uholanzi ulisema kombora aina ya Buk lililoundiwa Urusi lilitumiwa kutungua ndege hiyo.
Nani wa kulaumiwa?
Waasi walioungwa mkono na Urusi walilaumiwa na Ukraine na nchi za Magharibi na kudaiwa kutungua ndege hiyo 17 Julai 2014.
Wakati huo, wanajeshi wa Ukraine walikuwa kwenye vita vikali na waasi hao waliotaka kujitenga kwa maeneo ya mashariki mwa Ukraine.
Urusi imekana kuhusika na pia kupuuzilia mbali madai kwamba mtambo uliorusha kombora hilo la Buk ulikuwa maeneo ya Urusi.
Lakini baada ya kisa hicho, Umoja wa Ulaya (EU) na Marekani waliiwekea vikwazo Urusi.
Mapema wiki hii, Urusi ilitoa picha za mitambo ya rada, ambazo ilisema zinaonesha ndege hiyo haingetunguliwa na watu kutoka maeneo yaliyoshikiliwa na waasi.
Wakosoaji wa Urusi wanasema Urusi imetoa simulizi tatu tofauti kuhusu matukio yaliyojiri wakati wa kutunguliwa kwa ndege hiyo.
The Republican candidate for White House appeared to use an unusual adverb in his debate against Hillary Clinton. Or did he? Jon Kelly investigates.
There was a moment in the first US presidential debate when lots of people asked themselves: "Did Trump just say 'bigly'?"
Followed quickly by: "Is that even a word?"
It came during a discussion on fiscal policy, when, Donald Trump told his opponent: "I'm going to cut taxes bigly, and you're going to raise taxes bigly." Or so many thought, anyway.
Wagombea urais nchini Marekani Hillary Clinton na Donald Trump wamepambana vikali katika mdahalo wa kwanza wa televisheni ambapo wamepingana katika masuala mbali mbali ikiwemo masuala ya sera, kodi, ajira na uchumi.
Kadhalika wamejibizana kuhusu Vita vya Iraq na juhudi za kukabiliana na kundi linalojiita Islamic State.
Msimamizi wa mdahalo huo Lester Holt amemwuliza mgombea wa chama cha Republican Donald Trump mbona kufikia sasa bado hajaweza wazi taarifa zake za ulipaji kodi.
Mgombea wa chama cha Democratic Hillary Clinton amemshutumu mpinzani huyo wake akisema amekuwa akikwepa kulipa kodi na kudokeza kwamba hilo lina maana kwamba hakuwezi kuwa na wanajeshi, pesa za kulipa wanajeshi waliostaafu pamoja na kufadhili elimu na huduma ya afya.
Lakini tajiri huyo kutoka New York amejibu kwa kusema kwamba atatoa hadharani taarifa hizo iwapo Bi Clinton naye atakubali kutoa barua pepe 33,000 ambazo zilifutwa kutoka kwa sava yake wakati wa uchunguzi kuhusu tuhuma kwamba alitumia barua pepe ya kibinafsi kwa kazi rasmi alipokuwa waziri wa mambo ya nje wa Marekani.
Kundi la waasi nchini Sudan Kusini la Democratic Movement Cobra Faction, limetangaza kuwa litarejelea mapigano dhidi ya serikali ya Rais Salva Kiir.
Kundi hilo linaloongozwa na Luteni Khalid Botrus Bora, limekuwa likipagia haki zaidi za jamii ya Murle, na liliafikiana makubaliano ya amani na serikali ya Juba mwezi Mei mwaka 2014.
Katika taarifa, lilisema kuwa litajiunga na vikosi vingine ambavyo kwa sasa vinapiga na serikali.
Mtandao wa Sudan Tribune unaripoti kuwa tangazo hilo lililotolewa hii leo mjini Nairobi, Kenya, linajiri baada ya aliyekuwa waziri wa kilimo nchini humo Lam Akol, kuunda kundi jipya la waasi baada ya majuma kadha ya mazungumzo na makundi ya upinzani.
Mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yalizuka katika taifa hilo janga zaidi duniani mwezi Disemba mwaka 2013.
Image copyrightAFPImage captionAhmad Al Faqi Al Mahdi alikiri mashtaka
Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita (ICC) imemhukumu mwanamgambo wa Kiislamu raia wa Mali Ahmad Al Faqi Al Mahdi kifungo cha miaka tisa jela.
Al-Mahdi alikuwa ameshtakiwa makosa ya uhalifu wa kivita kuhusiana na kuharibiwa kwa makaburi tisa na msikiti mashuhuri katika mji wa kale wa Timbuktu, 2012.
Wakati wa kusikizwa kwa kesi yake, Al Faqi Al Mahdi alikiri mashtaka.
Kesi dhidi yake ilisikizwa siku chache tu kwa sababu yake kukiri mashtaka.
Mshtakiwa ni mwalimu wa kidini na anadaiwa kuamrisha wapiganaji wa kundi la Kiislamu la
Ansar Dine waharibu turathi na maeneo ya kidini Timbuktu kati ya 2012 na 2013.
Jumapili, 25 Septemba 2016
Image captionTrump atishia kumualika aliyekuwa mpenzi wa Clinton
Donald Trump ametishia kumualika mwanamke ambaye alikuwa mpenzi wa Bill Clinton akiwa kwenye ndoa na Hillary Clinton.
Trump amesema atamualika Gennifer Flowers akae mbele kabisa, kwenye mjadala baina yake Trump na mpinzani wake wa kugombea urais, Hillary Clinton, hapo kesho.
Bwana Trump alisema hayo, kujibu matamshi ya bilioneya anayeshindana naye, Mark Cuban ambaye alisema, kampeni ya Clinton imempa kiti cha mbele katika mjadala huo.
Image captionFabregas akimenyana na Alexis sanchez
Arsenal imepanda hadi nafasi ya tatu katika ligi ya Uingereza baada ya kucharaza Chelsea 3-0.
Alexis Sanchez alichukua fursa ya pasi mbaya iliopigwa nyuma na beki Gary Cahil katika lango la Chelsea kuiweka kifua mbele Arsenal.
Theo Walcot baadaye alifunga bao la pili baada ya Hector Bellerin kumpatia pasi nzuri ,kabla ya Mesut Ozil kufunga la tatu.
Chelsea walishindwa kujibu mchezo mzuri wa Arsenal na hawakufanikiwa kuitatiza Arsenal kutoka dakika ya kwanza hadi ya mwisho huku Batshuayi akikosa bao la wazi baada ya kusalia na Kipa alipoingia kama mchezaji wa ziada.