ADD THIS

https://www.facebook.com

Jumatatu, 3 Oktoba 2016

Tume: Uchaguzi DR Congo utafanyika 2018

Taarifa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, zinasema kuwa tume huru ya Uchaguzi nchini humo, imetangaza kuwa uchaguzi mkuu sasa utaandaliwa Novemba mwaka wa 2018 na wala sio mwaka huu kama ilivyotarajiwa.
Viongozi kadha wa upinzani walioshiriki katika mazungumzo ya amani ya kitaifa wameafikiana na uamuzi huo, lakini kuna wale wanaoupinga wakisema ni njama ya Rais Joseph kabila kusalia madarakani.
Image result for TUME YA UCHAGUZI DRC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni